Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 188 WIMBI LITAKASALO nyimbo za wokovu
1
Wimbi la damu ya Yesu
Linatutakasa;
Aliumia kusudi
Tupate uzima.
Wimbi la damu naona,
Naingia, natakaswa!
Bwana asifiwe sana,
Hutakasa, hutakasa.
2
Damu inasema kwangu,
Nasikia mvuto;
Inasema, moyo wangu
Hutakaswa nayo.
3
Naondoka kutembea
Kwa nuru ya mbingu;
Mavazi yamesafishwa;
Moyoni ni Yesu.
4
Neema ni ya ajabu,
Kutakaswa ndani!
Na kuwa naye Yesu tu,
Aliye Mwokozi.