Nyimbo Za Sifa
Wimbo 96 Kazi Yangu lkiisha. Maneno ya wimbo
Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka
Na kuvaa kutokuharibika
Nitamjua Mwokozi nifikapo ng’amboni
Atakuwa wa kwanza kunilaki
Chorus
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari
Furaha nitapata nikiona makao
Bwana aliyoyatuandalia
Nitamsifu Mwokozi kwa rehema na pendo
Vilivyonipa pahali Mbinguni
Nao waliokufa katika BwanaYesu
Nitawaona tena huko juu
Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni
Nataka kumwona Mwokozi kwanza
Milangoni mwa mji Bwana atanipisha
Pasipo machozi wala huzuni
Nitauimba wimbo wa milele, lakini
Nataka kumwona mwokozi kwanza