Nyimbo Za Sifa
Wimbo 3 Jina la Yesu, Salamu!. Maneno ya wimbo
jina la Yesu, salamu!
Lisujudieni,
Ninyi Mbinguni, hukumu
Na enzi mpeni
Enzi na apewe kwenu
Watatea dini
Mkuzeni Bwana wenu
Na enzi mpeni
Enyi mbegu ya rehema
Nanyi msifuni;
Mmeponywa kwa neema,
Na enzi mpeni.
Wenye dhambi kumbukeni
Ya Msalabani,
Kwa furaha msifuni
Na enzi mpeni
Kila mtu duniani
Msujudieni,
Kote-kote msifuni
Na enzi mpeni
Sisi na wao pamoja
Tu mumo sifani
Mile-Ie sifa ni moja
Ni “Enzi mpeni”.