Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 143 NAAMINI nyimbo za wokovu
1
Baba sina msaada
Ila kwako pekee;
Kama kwangu ungefichwa,
Nifanyeje, Baba?
Sasa hivi naamini
Yesu alikufa,
Aliimwaga damu yake,
Nitoke dhambini.
2
Naamini mwana wako
Nipe nguvu zako;
Nijazie mahitaji,
Katika saa hii.
3
Ni furaha gani kwangu
Kukuona uso!
Nijue sauti yako,
Nipate neema.