Nyimbo za wokovu
Wimbo 36 Mwokozi Alinifia Maneno ya wimbo
Mwokozi alinifia,
Yesu Mfalme wangu;
Akajitoa kabisa,
Kwa niaba yangu.
Mwokozi, nisaidie
Niwe mwaminifu;
Utakapomiliki juu,
Bwana, nikumbuke.
Aliugue mtini,
Kwa maovu yote;
Alikufa hapa chini,
Tuokoke sote.
Nijifiche uso wangu,
Nione msalaba;
Nimpe shukrani yangu,
Astahili sifa.
Sina uwezo kulipa,
Deni ya upendo;
Bali Yesu, najitoa,
Nitumike kwako.