Nyimbo za wokovu
Wimbo 167 Kibarikiwa Kifungo Maneno ya wimbo
Kibarikiwe kifungo
Kitufungiacho mioyo,
Ushirika wetu wa fikira zetu
Ni kama ule wa mbingu.
Mbele ya enzi ya Baba,
Dua zetu twaziomba;
Hofu zetu na matumaini yetu,
Hayo ni mamoja kwetu.
Huzuni zetu twashika,
Na mizigo yetu pia;
Ndani yao yote twashirikiana
Hata katika kulia.
Tutawanyikapo mbali,
Hiyo yatufadhisha;
Lakini tungali pamoja rohoni
Hata tutakutanika.