Nyimbo Za Sifa
Wimbo 6 Ni Tabibu wa Karibu. Maneno ya wimbo
Ni taibu wa karibu;
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima;
Ni dawa yake njema
Chorus
Imbeni, malaika
Sifa za Yesu Bwana
Pweke limetukuka
jina lake Yesu
Hatufai kuwa hai,
Wala hatutumai,
llaYeye kweli ndiye
Atupumzishaye.
Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia;
Twenendeni na amani
Hata kwake Mbinguni.
Huliona tamu jina
LaYesu Kristo Bwana
Yuna sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa
Kila mume asimame
Sifa zake zivume
Wanawake na washike
Kusifu jina Iake
Na vijana wote tena,
Wampendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake