Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 56 WAPONYENI WATU nyimbo za wokovu
1
Walio kifoni, nenda waponye,
Uwatoe walio shimoni;
Wanaoanguka uwainue;
Habari njema uwajulishe.
Walio kifoni waokoeni,
Mwokozi yuko huwangojea.
2
Wajapokawia anangojea,
Awasubiri waje tobani;
Mwokozi hawezi kuwadharau,
Huwasamehe tangu zamani;
3
Na ndani ya moyo wa wanadamu
Huwamo shida, tena huzuni;
Lakini kwa Yesu kuna rehema
Kuwaponya na kuwaokoa.
4
Walio kifoni, nenda waponye
Kazi ni yetu, zawadi iko;
Nguvu kuhubiri Bwana hutoa
Kwa subira tuwavute sasa