Nyimbo za wokovu
Wimbo 181 Fedha Wala Dharau Maneno ya wimbo
Fedha wala dhahabu hazitosheki,
Kuninunulia wokovu wangu;
Damu ya Msalaba ndiyo ni msingi,
Kifo cha Mwokozi kimetosheka.
Nakombolewa, si kwa fedha,
Wala si kwa dhahabu;
Bei aliyoninunulia
Ni damu yake Yesu.
Fedha wala dhahabu hazitosheki,
Amri za Mungu zilinikataza;
Damu ya Msalaba ndiyo ni msingi,
Kifo cha Mwokozi hunituliza.
Fedha wala dhahabu hazitosheki,
Kuinunu njia ya uzima;
Damu ya Msalaba ndiyo ni msingi,
Kifo cha Mwokozi huleta raha.