Nyimbo za wokovu
Wimbo 180 Karibu Nawe, Ee Mwokozi Maneno ya wimbo
Karibu nawe, Ee Mwokozi,
Univute Bwana wa thamani;
Unikaribishe Moyoni,
Uniweke kwako salamani,
Uniweke kwako salamani.
Karibu nawe, sina kitu,
Sikuiletea sadaka kuu;
Nakujitolea kabisa,
Kwa damu nipate kutakaswa,
Kwa damu nipate kutakaswa.
Karibu nawe, Bwana wangu,
Niliuacha uovu wangu;
Kiburi changu na anasa,
Namtaka Yesu aliye Bwana,
Namtaka Yesu aliye Bwana.
Karibu nawe, hata mwisho,
Nina salama ndani ya Kristo;
Mwokozi wangu kwa milele,
Nitakuwa karibu na wewe,
Nitakuwa karibu na wewe.