Nyimbo Za Sifa
Wimbo 118 Bwana Yesu Atakuja. Maneno ya wimbo
Bwana Yesu atakuja, Vumilia!
Omba, ukiwa na haja, Vumilia!
Mbinguni Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako,
Nawe utatika huko, Vumilial
Ikikucheka dunia, Vumilia!
Mwovu atakuvizia, Vumilia!
Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda
Roho yako akupenda, Vumilia!
Na ukiwa hatarini, Vumilia!
Dhiki nyingi duniani, Vumilia!
Vyatupasa kuyakuta Majaribu na matata,
Na Bwana hakutuficha, Vumilia!
Adui wakikutana, Vumilia!
Na ndungu wakikukana, Vumilia!
Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutish·a
Mungu chini atashusha; Vumilia!
Moyoni una majonzi, Vumilia!
Ndiyo bonde-ya-machozi Vumilial
Hima, tutaandamana Kwetu Mbinguni na Bwana.
Tena hatutaachana; Vumilia!