Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 37 PENDO LAKO, EE MWOKOZI nyimbo za wokovu
1
Pendo lako, Ee Mwokozi,
Hushinda pendo zote!
Kaa nasi, ndani yetu,
Furaha ya mbinguni.
Yesu, u rehema tupu,
Safi, na kusamehe,
Mfariji mwenye huzuni
ziondoe machozi.
2
Roho yako ya upendo
Tuma kwa kundi lako;
Hebu tuirithi raha, Iliyoahidiwa.
Uondoe moyo mbaya,
U Mwanzo, tena Mwisho;
Timiza imani yetu,
Ili tuwekwe ‘huru’
3
Yesu, uje kwetu sasa,
Tupokee huruma;
Rudi kwetu, tena
kamwe Usituache pekee.
Tungekutukuza leo,
Pamoja na malaika,
Imba na kutoa sifa,
Ingia kwa ibada.
4
Sasa, Bwana, kazi yako,
Imalize moyoni;
Takasa hekalu lako,
Wokovu kamilisha!
Safisha viumbe vyako
katika wakati huu;
Tupumzike toka dhambi,
Tuingie mbinguni;