Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 28 JINA LA THAMANI nyimbo za wokovu
1
Jina Lake Yesu tamu,
Lihifadhi moyoni;
Litakufariji ndugu,
Enda nalo po pote.
Jina la Thamani,
(Thamani) (Thamani)
Tumai la dunia
Jina la Thamani
Furaha ya mbinguni.
2
Jina la Yesu lafaa
kama ngao vitani.
Majaribu yakisonga,
Omba kwa jina hili.
3
Jina hili la thamani
Linatufurahisha,
Anapotukaribisha,
Na tunapomwimbia.
4
Mwisho wa safari yetu
Tutakapo msujudu,
Jina hili tutasifu
Furaha ya mbinguni.