Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 181 TUTAKAA MAHALI PA MAJI nyimbo za wokovu
1
Mahali pa maji mazuri
Maji ya uzima;
Anapotungojea Yesu
Tutakaribishwa.
Mahali pa maji mazuri,
Penye maji ya uzima;
Tutakaa na Mwokozi,
Chemchemi ya uzima.
2
Tunapochoka safarini
Tamu kupumzika.
Panapo maji ya uzima
Yatufurahisha.
3
Una kiu? uje kwa Yesu,
Utaburudishwa;
Yesu yu maji ya uzima,
Unywe, uokoke.