Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 144 NI WAKO BWANA nyimbo za wokovu
1
Ni wako Bwana, Ninasikia,
Unaponena nami,
Lakini kweli nataka kwako
nizidi kusongea.
Bwana vuta, (vuta) Nije nisonge,
Sana kwako mtini,
Bwana vuta, vuta, Nije nisonge,
Kwa damu ya thamani.
2
Niweke sasa, Nikatumike,
Kwa nguvu za neema,
Uyapendayo nami nipende
nizidi kukwandama.
3
Nina furaha, Tele kila saa,
Nizungumzapo nawe,
Ninanena kama kwa rafiki
nikipiga magoti.