Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 138 NITAKUANDAMA KOTE nyimbo za wokovu
1
Nitakuandama Kote,
Nitakapoagizwa,
Wewe ukiniongoza
Nami nitaandama.
Nitakuandama kote,
Naam, ulinifia;
Kwa neema yako Bwana
Napenda kuandama.
2
Njia ijapoparuza
Kwa miiba na fujo,
Ulitangulia mbele
Nami nitaandama.
3
Nijapokuta taabu
Na majaribu kote,
Nakumbuka shida yako,
Nami nitaandama.
4
Nijapoona ukiwa
Na mateso makali
Wewe uliyatikiza
Nami nitaandama.
5
Ijapo wanipeleka
Vilindini mwa giza,
Wewe uliyatikiza
Nami nitaandama.