Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 114 YESU NATAKA KUTAKASWA SANA nyimbo za wokovu
1
Yesu Mwokozi ili nitakaswe,
Nataka moyo uwe enzi yako.
Ukiangushe kilichoinuka
unioshe sasa niwe mweupe.
Mweupe tu, ndiyo mweupe,
Ukiniosha nitakuwa safi.
2
Bwana Yesu sasa unitazame,
unifanye niwe dhabihu hai.
Najitoa kwako, na moyo, vyote;
unioshe sana niwe mweupe.
3
Bwana kwa hivyo nakuomba sana,
nakungojea miguuni pako
Wanaokuja hutupi kamwe,
unioshe sasa niwe mweupe.