Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 107 NIPO BWANA, NITUME nyimbo za wokovu
1
Sauti ni yake Bwana,
Kwenda, nani tayari?
Mavuno yanakawia,
Nani atayavuna?
Kwa kudumu anaita
Zawadi atatoa;
Nani atakaye jibu
Nipo Bwana nitume
2
Kama huwezi safari
Hata nchi za mbali,
Pana watu karibuni
Wasiomjua Yesu;
Kama huwezi kusema
Jinsi ya malaika,
Waweza kuutangaza
Upendo wa mwokozi.
3
Ingawa huwezi kuwa
Mkesha mlangoni,
Ukiwatolea watu
Nafasi ya uzima ;
Kwa sala na kwa sadaka
Watoa msaada
Kama Harun mwaminifu
Kuinua mikono
4
Roho za watu zikifa
Bwana akikuita ,
Usiseme kwa uvivu,
Hakuna kazi kwangu.
Kwa furaha anza kazi
Ile aliokupa,
Ukajibu mara moja
Nipo Bwana, nitume.