Nyimbo Za Sifa
Wimbo 113 Bwana Yesu. Maneno ya wimbo
Bwana Yesu, Bwana Yesu
Mbona unaumia? Unateseka sana
Kwa ajili ya kuomba
Waomba na jasho jingi Iikageuka damu
Chorus
Kumbe! ni dhambi zangu zinazokuumiza
Bwano wangu, Mungu wangu
Mimi Ieo, naja kwako
Ili niziungame
Bwana.Yesu, Bwana Yesu
Mbona unaumia na mizigo mizito?
Umejitwalia Wewe msalaba mabengani
Kwa ajili ya watu
BwanaYesu, BwanaYesu
Mbona unatukanwa, wawambwa kama mwizi
Bila tusi ukalia, Baba wangu, wasamehe
Chukua roho yangu
BwanaYesu, Bwana Yesu
Muda ulipofikia, nchi ikawa giza
Mbinguni pakatulia, angani pakawa kimya
Watu wakaogopa
BwanaYesu, BwanaYesu
jinsi ulivyoumwa, ukamwomba Baba
Leo umeshinda kifo, sasa wapaa Mbinguni
Naimba, Haleluya