Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 58 ZITAKUWA NYOTA TAJINI? nyimbo za wokovu
1
Leo ninafikiri
Ya nchi nzuri
Ninayotaka kuiona:
Nisimamapo karibu
Na Mwokozi,
Tajini zitakuwa nyota?
Sijui tajini mwangu
Kama nyota
Zitang’aa kila wakati!
Nitakapoamka
Katika majumba.
Zitakuwa nyota tajini?
2
Kwa nguvu za Bwana
Nitafanya kazi,
Nitavuta roho za watu,
Ili niwe na nyota katika taji,
Bwana anapotupa tunu.
3
Nitakuwa na furaha
Nikimwona,
kuweka miguuni pake
Watu waliovutwa
Kwa ajili ya
Kazi yangu na Roho yake.