Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 218 OMBA SANA ASUBUHI nyimbo za wokovu
Omba sana asubuhi,
Omba sana mchana,
Omba sana na jioni,
Bwana hutusikia.
Mungu hujibu maombi,
Asubuhi na mchana,
Hata hutungojea tena,
Wakati wa jioni.
Na tuimbe asubuhi,
Tena saa za mchana,
Hivi tutafurahi Naye,
Pumziko la jioni.