Nyimbo za wokovu
Wimbo 50 Huniongoza Mwokozi Maneno ya wimbo
Huniongoza Mwokozi,
Ndipo nami hufurahi,
Niendapo pote napo,
Ataniongoza papo.
Kuongoza hunishika;
Kwa mkono wa hakika;
Nitaandamana naye
Kristo aniongozaye
Pengine ni mashakani
Nami pengine rahani;
Ni radhi, ijayo yote,
Yupo nami siku zote.
Mkono akinishika
Kamwe sitanung`unika:
Atakachoniletea
Ni tayari kupokea.
Nikiisha kazi chini
Takwenda huko mbinguni,
Nako nitamtukuza
Kristo aliyeongoza.