Nyimbo za wokovu
Wimbo 208 Kwake Yesu, Nakaa Salamani Maneno ya wimbo
Kwake Yesu, nakaa salamani,
Ijapokuwa giza na shida;
Nitamwamini, atanihifadhi,
Amenikomboa niwe wake.
Kwake Yesu, kwake Yesu,
Sitajitenga na Yeye;
Kwake Yesu, hapo nadumu,
Kwa salama ya milele.
Kwake Yesu, ninalo kimbilio,
Wakati nionapo huzuni;
Ataniponya nisifadhaike,
Nitakaa naye salamani.
Kwake Yesu iko fuhara tele,
Nitaishi naye mpaka mwisho;
Atanilinda, sitashindwa kamwe,
Hunipa baraka na pumziko.