Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 78 MPAKA LINI BWANA? nyimbo za wokovu
1
Mpaka lini Bwana,
Utakaa mbali?
Kumetuchosha moyo,
Kukawia hivi.
Utatujia lini,
Ili tufurahi
Katika ile nuru,
Kuja kutukufu?
2
Mpaka lini Yesu,
Utaacha watu
Uliowakomboa,
Wawe na mashaka?
Wachache waamini,
Kwamba utarudi;
Wachache wa tayari,
Bwana kukulaki.
3
Waamshe watu wako,
Tangaza kilio;
Mwe watakatifu,
Bwana yu karibu!
Utatujia lini,
Ili tufurahi
Katika ile nuru,
Kuja kutukufu?