Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 45 MWANGA UMO MOYONI nyimbo za wokovu
1
Mlimani pana mwanga,
Mwanga wa jua zuri
Shambani na baharini
Jua tukufu liko;
Mwanga ulio mkubwa
Umo moyoni mwangu
Kwa kuwa Yesu alipo
Hapa pana mwangaza.
Mwangaza ulio nzuri.
Mwanaga umo moyoni;
Akiwapo Bwana Yesu
Pana Mwanga moyoni.
2
Kama mavazi kikuu
Ninavua huzuni;
Nguo nzuri za furaha
Umenipa zakuvaa.
Nakuandama rohoni
Hata nyumba ya juu
Iliyopambwa vizuri
Katika pendo lako.
3
Ulinikomboa Yesu;
Maisha yangu, mali,
Vyote ni vyako, Mwokozi
Daima nikusifu.
Nakuandama rohoni
Hata nyumba ya juu
Iliyopambwa vizuri
katika pendo lako.