Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 204 YA SABA NI KWA YESU nyimbo za wokovu
1
Siku sita fanya kazi,
Ya saba ni kwa Yesu.
Hapo tunapopumzika,
Kwani ni yake Yesu.
Moja, mbili, tatu, nne,
tano, sita, zote kwetu;
Lakini tutakumbuka,
Ya saba ni kwa Yesu!
2
Huonyesha ya kufanya,
Kwa kuwa ni ya Yesu,
Na atuonyesha njia,
Tutamfuata Yesu.
3
Tuombe kila Sabato,
Na kujifunza kwake;
Tutamtii daima,
Tutakaa na Yesu.