Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 116 MOYO SAFI nyimbo za wokovu
1
Bwana ninataka hili,
kwa kuwa nimechafuka,
Kwa moto au kwa maji
unisafishe kabisa.
Unisafishe Mwokozi ndani,
na nje kwa moto
Utakavyo:ili dhambi
ife kwangu, ife kwangu.
2
Kupewa hekima yote,
itakuwa tunu kubwa;
Lakini moyo safi ni,
bora kwangu, bora kwangu!
3
Mpaka moyo ni safi
siwezi kuyafahamu
Mambo mazuri ya mbingu,
mambo mazuri ya mbingu.