Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 113 BUBUJIKO nyimbo za wokovu
1
Damu imebubujika,
Ni ya Imanweli,
Wakioga wenye taka,
Husafiwa kweli.
2
Ilimpa kushukuru
Mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru,
Yanisafi ndani.
3
Kondo-o wa kuuawa,
Damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa
Kwa utimilivu.
4
Bwana, tangu damu yako
Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako,
‘Taimba milele.
5
Bwana, umenikirimu
Nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu
Ya mali ya kweli.
6
Nikubali kukwimbia
Mbinguni milele.
Mungu nitamsifia
Jina lako pweke.