Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 79 NATAKA IMANI HII nyimbo za wokovu
1
Nataka imani hii.
Imani imara
Ambayo haitetemi Kitu chote
Wakati wa shida,
Wakati wa shida.
2
Isiyonung’unikia
Huzuni, taabu;
Lakini katika saa ya matata
Humwamini Mungu,
Humwamini Mungu.
3
Imani inayong’aa
katika tufani;
Isiyoogopa giza, wala shida,
Njaa na hatari,
Njaa na hatari.
4
Haiogopi dunia,
Kudharau kwake;
Haiangushwi na hila, na uongo
Dhambi na ogofyo,
Dhambi na ogofyo.
5
Bwana, nipe imani hii,
Hivi nitaweza
Kuonja hapa chini Ulimwengu,
Kurithi furaha,
Kurithi furaha.