Nyimbo za wokovu
Wimbo 2 Jina La Yesu, Salamu! Maneno ya wimbo
Jina la yesu, salamu!
Lisujudieni,
Ninyi mbinguni hukumu
Na enzi mpeni.
Enzi na apewe kwenu,
watetea dini
Mkuzeni Bwana wenu
Na enzi mpeni
Enyi mbegu ya rehema
Nanyi msifuni;
Mmeponywa kwa neema,
Na enzi mpeni
Wenye dhambi kumbukeni
Ya Msalabani
Kwa furaha msifuni
Na enzi mpeni
Sisi na wao pamoja
Tu mumo sifani
Milele sifa ni moja,
Ni Enzi mpeni.