Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 155 NJIANI HUNIONGOZA nyimbo za wokovu
1
Njiani huniongoza
Yesu wangu, Mwokozi:
Rehema hatapunguza,
Milele Kiongozi.
Ina raha kwandamana
Duniani daima:
Nijaposumbuka sana,
Yeye hutenda vyema.
2
Njiani huniongoza
Hupunguza matata;
Nikiugua hupoza,
Na njaani nashiba.
Lichokapo guu langu
Nguvu zikapungua,
Jiwe lilo mbele yangu
Hunibubujika.
3
Njiani huniongoza
Kwa pendo zilizo kuu,
Mwisho atanituliza
Kwake Baba yangu juu.
Nikivikwa kutokufa,
Nikae na Mwokozi,
Nitamsifu sana; sifa:
Kweli ni Kiongozi