Nyimbo Za Sifa
Wimbo 123 Sauti Sikilizeni. Maneno ya wimbo
Sauti sikilizeni
Za waimbao juu
“Aleluya, Aleluya.
Aleluya, Mkuu!”
Wako makundi-makundi
Kama nyota wang’ara.
Kwa makuti ya mitende.
Na meupe wamevaa.
Wazazi na manabii
Wafanyaji wa njia;
Mashahidi, waandishi,
Nao wafalme pia!
Mabikira, kina-mama,
Wajane wa kusali,
Waimba wakikutana
“Msifu Imanweli.”
Watu toka huzunini
Wameosha na nguo,
Ni kwa damu yake Yesu,
Maonjo, mbali. nao!
Walitekwa, wakikatwa
Hata kwa misumeno,
Kwao kifo na Shetani
Walishindiwa mno.
Mungu mumo mwake
Mungu,
Nuru mumu mwa nuru,
Kwa kufungamana mwako
Tutaishi mahuru;
Tujalize, Imanweli,
Kujaa kwako Wewe
Mungu Baba, Mungu
Mwana,
Mungu Roho, tunawe.