Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 91 KAA NAMI nyimbo za wokovu
1
Kaa nami, ni usiku tena;
Usiniache gizani, Bwana
Msaada wako haukomi;
Nili peke yangu, kaa nami.
2
Siku zetu hazikawi kwisha;
Sioni la kunifurahisha;
Hakuna ambacho hakikomi,
Usiye na mwisho kaa nami.
3
Nina haja nawe kila saa:
Sina mwingine wa kunifaa
Mimi nitaongozwa na nani
Ila wewe? Bwana kaa nami.
4
Sichi neno uwapo karibu;
Nipatalo lote, si taabu;
Kifo na kaburi haviumi;
Nitashinda kwako, kaa nami.
5
Nilalapo nikuone wewe,
Gizani mote nimulikiwe;
Nuru za mbinguni hazikomi,
Siku zangu zote; kaa nami.