Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 115 NAENDEA MSALABA nyimbo za wokovu
1
Naendea msalaba,
Ni mnyonge, mpofu,
Yapitayo naacha
Nipe msalaba tu.
Nakutumaini tu,
Ewe Mwana wa Mungu;
Nainamia kwako,
Niponye sasa, Bwana.
2
Nakulilia sana;
Nalemewa na dhambi;
Pole Yesu asema:
Nitazifuta zote
3
Natoa vyote kwako,
Nafasi nazo nguvu,
Roho yangu na mwili
Viwe vyako milele.
4
Kwa damu yake sasa
Amenivuta sana,
Upendo hubidisha,
Nimtafute Mwokozi.