Nyimbo za wokovu
Wimbo 8 Nitaimba Juu Ya Mkombozi Maneno ya wimbo
Jina lake yesu tamu.
Tukilisikia
Hutupoza tena hamu,
Hutuondolea.
Roho iliyoumia
Kwalo hutibika,
Chakula njaani pia;
Raha, tukichoka Jina hili ni msingi,
Ngao, ngome, mwamba,
Kwa hili napata ungi,
Kwangu ni akiba.
Yesu, Mchunga, Rafiki,
Mwalimu, kuhani,
Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki,
Uzima kifoni.
Moyo wangu hauwezi,
Kukusifu kweli,
Ila sifa zangu hizi,
Bwana zikubali.
Na utakaponiita,
Kuja kwako Bwana,
Huko kwako sitaacha,
Kukusifu sana.