Nyimbo za wokovu
Wimbo 76 Nionapo Amani Kama Shwari Maneno ya wimbo
Nionapo amani kama shwari,
Au nionapo shida;
Kwa hali zote umenijulisha
Ni salama rohoni mwangu.
Salama rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.
Ingawa shetani atanitesa,
Nitajipa moyo kwani
Kristo ameona unyonge wangu
Amekufa kwa roho yangu.
Dhambi zangu zote, wala si nusu,
Zimewekwa Msalabani;
Wala sichukui laana yake,
Ni salama rohoni mwangu.
Ee Bwana, himiza siku ya kuja,
Panda itakapolia;
Utakaposhuka sitaogopa,
Ni salama rohoni mwangu.