Site icon Treasure Hymns- Swahili

Wimbo 19 Kaa Nami Maneno ya wimbo

Nyimbo za wokovu

Wimbo 19 Kaa Nami Maneno ya wimbo

 

Kaa nami ni usiku tena;
Usiniache gizani, Bwana:
Msaada wako haukomi;
Nili peke yangu, kaa nami.

Siku zetu hazikawi kwisha,
Sioni la kunifurahisha;
Hakuna ambacho hakikomi,
Usiye na mwisho, kaa nami

Nina haja nawe kila saa;
Sina mwingine wa kunifaa;
Hakuna ambacho hakikomi,
Usiye na mwisho, kaa nami.

Nina haja nawe kila saa;
Sina mwingine wa kunifaa;
Mimi nitaongozwa na nani
Ila wewe? Bwana, kaa nami.

Sichi neno uwapo karibu;
Nipatalo lote, si taabu;
Kifo na kaburi haviumi;
Nitashinda kwako, kaa nami.

Nilalapo nikuone wewe,
Gizani mwote nimulikiwe;
Nuru za mbinguni hazikomi,
Siku zangu zote kaa nami.

Exit mobile version