Site icon Treasure Hymns- Swahili

Wimbo 176 Kutoka Dhambini Maneno ya wimbo

Nyimbo za wokovu

Wimbo 176 Kutoka Dhambini Maneno ya wimbo

 

Kutoka dhambini mpaka mbingu,
nimeshikwa na pendo la Mungu;
Kwa vifungoni nimeondoka,
Na Yesu hunishika.

Yesu hunishika,
Yesu hunishika;
Kutoka gizani mpaka mwanga,
Na Yesu hunishika.

Kutoka taabu mpaka raha,
Nimefika nchi ya Baraka;
Kwa fahari yake nitakaa,
Na Yesu hunishika.

Kwa kujitoa nitamwabudu,
Kwa pendo lake nitamshukuru;
Kwa milele naye nitakaa,
Na Yesu hunishika.

Exit mobile version