Site icon Treasure Hymns- Swahili

Wimbo 104 Ni Mwokozi Aliyenifia Maneno ya wimbo

Nyimbo za wokovu

Wimbo 104 Ni Mwokozi Aliyenifia Maneno ya wimbo

 

Ni Mwokozi aliyenifia,
Nitoke dhambini, alisema,
Yeye aliyemwamini Mwana,

Anao uzima.

Amini, Amini, nakuambia,
Amini, Amini, ujumbe mpya;
Yeye aliyemwamini Mwana,

Anao uzima.

Dhambi zangu zilichukuliwa,
Deni zangu zote zililipwa;
Wote waliomwamini Mwana,

Wanao uzima.

Ijapo ningekuwa maskini,
Ijapo ningekuwa mkosaji;
Neno la furaha la Mwokozi,
Ninao uzima.

Na sina shaka, nitamwamini,
Yeye ajaye kwake hatupwi;
Amwaminiye, tuma habari.

Tunao uzima.

Exit mobile version