Nyimbo Za Sifa
Wimbo 2 Nilikuwa Kondoo Aliyepotea. Maneno ya wimbo
Nilikuwa kondoo aliyepotea
Sikupenda zizi kamwe, ila kutembea
Nilikuwa mwana asiyesikia
Sikupenda Baba yangu wala kutulia
Na Mchunga Mwema alinitafuta
Baba kwa mapenzi ndiye aliyenivuta
Karibu ya kufa kwa kiu na kwa njaa
Waliniona mnyonge, waliniokoa
Yesu ni Mchunga, mwenziwe hapana
Aliosha taka zangu, dhambi nyingi sana
Kwa vidonda vyangu alicia dawa
Ndiye ahyenipata, na kwake nalindwa
Nilikuwa kondoo aliyepotea
Sasa nampenda Baba, na Mchunga pia
Kwanza nilitanga na kukosa sana
Hivi nyumbani mwa Baba sipotei tena.