Nyimbo Za Sifa
Wimbo 2 Mwamba Wenye lmara. Maneno ya wimbo
Mwamba wenye imara
Kwako nitaji?cha!
Maji hayo na damu
Yaliyotoka humu
Hunisafi na dhambi
Hunifanya mshindi
Kwa kazi zote pia
Sitimizi sharia
Nijapofanya bidii
Nikilia na kudhii
Hayaishi makosa
Ndiwe wa kuokoa
Sina cha mkononi
Naja Msalabani
Nili tupu, nivike
Ni mnyonge, nishike
Nili mchafu naja
Nioshe nisijafa
Nikungojapo chini
Nakwenda kaburini
Nipaapo Mbinguni
Na kukwona enzini
Roho yangu na iwe
Rahani mwako wewe