Nyimbo Za Sifa
Wimbo 154 Twimbe Wake na Waume. Maneno ya wimbo
Aleluya! Aleluya! Aleluya!
Twimbe wake na waume
Ndiye wa mbingu Mfalme
Ameshinda kifo Yesu, AleIuya
Asubuhi ya Pasaka
Wanawake wakatoka
Wamwone alikowekwa, Aleluya
Hao ndio wamekaa
Malaika wamevaa
Nguo zilozozagaa, Aleluya
Wakawauliza. “Kwani
Kumtafuta ufuni
Naye yu hai, jueni,Aleluya
“Akali kwa watu wake
Kumbukeni neno lake
Ni la kufufuka kwake, Aleluya
“Nami ndimi Mwanadamu
Watu watanihukumu
Ha sikai kuzimu, AleIuya
“Kwa wanangu muwasili
Waambieni na hili
Tutaonana Galili, Aleluya
Aleluya! Aleluya! Aleluya!
Usiku waikutana
Kwa hofu, akaja Bwana
“Ni amani” akanena,Aleluya
Thoma aliposikia
Hilo aliwaambia
Ni sharti kumwangalia,Aleluya
“Ati! Thoma huzioni
jeraha za mikononi
Miguuni, ubavuni?”, Aleluya
Mara akasujudia
Kwa imani akanena
“Bwana wangu, Mungu tena!,Aleluya
Kweli wongofu ni wao
Hao waamaniao
Heri kama waonao,Aleluya
Ni siku bora ya shani
Nanyi kwa Mungu imbeni
Za sifa na shukurani,Aleluya