Nyimbo Za Sifa
Wimbo 13 Cha kutumaini Sina. Maneno ya wimbo
Cha kutumaini sina
Ila damu yake Bwana
Sina wema wa kutosha
Dhambi zangu kuziosha
Chorus
Kwake Yesu nasimama
Ndiye Mwamba: ni solama
Ndiye Mwamba: ni salama
Njia yangu iwe ndefu
Yeye hunipa wokovu
Mawimbi yakinipiga
Nguvu zake ndiyo nanga
Damu yake na sadaka
Nategemea daima
Yote chini yakiisha
Mwokozi atanitosha
Nikiitwa hukumuni
Rohoni nina amani
Nikivikwa haki yake
Sina hofu mbele zake.