Site icon Treasure Hymns- Swahili

Wimbo 112 Enyi Wanadamu. Maneno ya wimbo

Nyimbo Za Sifa

Wimbo 112 Enyi Wanadamu. Maneno ya wimbo

 

Enyi wanadamu mbona
Sana mwatanga-tanga,
Kama kondoo wanyonge,
Wasio na mchunga?
Yuko Mchunga Mmoja
Mwenye mapenzi mama;
Haya kutaneni kwake,
Atawachunga vyema.

Mungu tunamwona kuwa
Mwenye uwezo wote;
Na nguvu zake zapita
Mawazo yetu yote;
Ni Baba, mapenzi yake
Ni makubwa hakika;
Hatuwezi kuyajua
Na hayana mpaka.

Rehema za Mungu nazo
Zina upana sana;
Kama huo wa bahari,
Mwisho wake hapana;
Haki yake ina mema.
Kwa hayo twashukuru,
Kwetu uko msamaha
Furaha na uhuru.

Mapenzi yake mapana,
Slsi hatuna cheo
Cha kutosha, nao moyo
Una wema upeo;
Ukombozi mwingi mno
Katika damu yake;
Sote twapata furaha
Kwa maumivu yake.

Yesu mkaribieni
Njoni kwaka kwa imani,
Mama yake ni hayo
Heri tuwa kama wana
Tushike neno Iake.
Daima atatujaza
Tele furaha yake.

Exit mobile version