Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 89 ASUBUHI nyimbo za wokovu
1
Bwana asubuhi kucha
Nitakuinua
Sauti yangu kuomba,
Nipate Baraka.
2
Nakuomba roho yako
Niongozwe nayo;
Nifanye yanipasayo,
Na mapenzi yako.
3
Wanaokutegemea,
U Mlinzi wao;
Matumaini wanayo,
Utayatimiza.
4
Na kwa wingi wafadhili,
Nyumbani mwako juu
Nitaingia na wimbo,
Pale kusujudu.