Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 69 CHA KUTUMAINI SINA nyimbo za wokovu
1
Cha kutumaini sina
ila damu yake Bwana,
Sina wema wakutosha,
Dhambi zangu kuziosha.
Kwake Yesu nasimama,
Ndiye Mwamba; ni salama;
Ndiye Mwamba; ni salama.
2
Njia yangu iwe ndefu
yeye hunipa wokovu;
Mawimbi yakinipiga
nguvu zake ndiyo nanga.
3
Damu yake na sadaka
nategemea daima,
Yote chini yakiisha
Mwokozi atanitosha.
4
Nikiitwa hukumuni,
Rohoni nina amani;
Nikivikwa haki yake
sina hofu mbele zake.