Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 52 NIPE BIBLIA nyimbo za wokovu
1
Nipe Biblia nyota ya furaha,
wapate nuru wasafirio;
Hakuna la Kuzuia amani,
Kwani Yesu alituokoa.
Nipe Biblia neno takatifu,
Nuru yake itaniongoza;
Sheria na ahadi na upendo,
hata mwisho vitaendelea.
2
Nipe Biblia nihuzunikapo
ikinijaza moyoni dhambi;
Nipe neno zuri la Bwana Yesu,
Nimwone Yesu Mwokozi wangu.
3
Nipe Biblia nipate kuona,
Hatari zilizo duniani;
Nuru ya neno lake Bwana Yesu,
Itaangaza njia ya kweli.
4
Nipe Biblia taa ya maisha;
Mfariji tunapofiliwa;
Unionyeshe taa ya mbinguni,
Nione utukufu wa Bwana.