Site icon Treasure Hymns- Swahili

Wimbo 18 MWOKOZI, KAMA MCHUNGA nyimbo za wokovu

Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns

Wimbo 18 MWOKOZI, KAMA MCHUNGA nyimbo za wokovu

 

1
Mwokozi, kama mchunga
Utuongoze leo;
Ututume malishoni;
Fanya tayari boma.
Bwana Yesu, peke yako
Umetuvuta kwako.

2
Tu wako, uwe rafiki,
Uwe mlinzi wetu;
Kundi lako ulilinde,
Tusivutwe na dhambi;
Bwana Yesu, tusikie,
Tukiomba, samehe.

3
Umetuahidi kwamba
Utakubali watu,
Utawahurumia na
Utawapa neema;
Bwana Yesu, tunapenda
Kuwa wako, mapema.

Exit mobile version