Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 151 HUNIONGOZA MWOKOZI nyimbo za wokovu
1
Huniongoza Mwokozi,
Ndipo nami hufurahi,
Niendapo pote napo,
Ataniongoza papo.
Kuongoza hunishika;
Kwa mkono wa hakika;
Nitaandamana naye
Kristo aniongozaye.
2
Pengine ni mashakani
Nami pengine rahani;
Ni radhi, ijayo yote,
Yupo nami siku zote.
3
Mkono akinishika
Kamwe sitanungunika;
Atakachoniletea
Ni tayari kupokea.
4
Nikiisha kazi chini
Sitakimbia mauti;
Kushinda ni ya hakika
Nikiongozwa na Baba.