Nyimbo Za Kristo – Swahili SDA Hymns
Wimbo 135 SAA HERI YA MAOMBI nyimbo za wokovu
1
Saa heri ya maombi,
Sasa kwako tunarudi,
Sumbuku ya kuondoa,
Shida zetu na pungufu.
Taabuni mara nyingi,
Roho zetu zimepona,
Mashakani tumeshinda,
Wakati wa saa tamu.
2
Saa heri ya maombi,
Twapeleka dhiki zetu
Kwake aliyeahidi
Kubariki wenye haja.
Huagiza tumwendee,
Tutegemee neno lake,
Hivyo tumwekee yote,
Wakati wa saa tamu.
3
Saa heri ya maombi,
Tutazidi kuingia,
Bomani mwetu
Na ngome,
Hata tuishapo mwendo,
Yesu atatusikia,
Tutamtafuta daima,
Na tutakapokutana,
Tutamwona saa tamu.